Nenda kwa yaliyomo

Lango:Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Milango ya Wikipedia: Sanaa · Utamaduni · Jiografia · Afya · Historia · Hisabati · Sayansi · Falsafa · Dini · Jamii · Teknolojia

hariri  fuatilia  

Lango la Afrika

Afrika ni bara la pili duniani kwa ukubwa, likiwa na eneo la kilometa za mraba zipatazo 30,370,000 na kwa idadi ya wakazi, hao wakiwa 1,225,080,510 (mwaka 2016). Asia ndiyo bara pekee la kushinda Afrika.

Neno "Afrika" limetokana na lugha ya Kilatini ya Roma ya Kale. Waroma kwa jina hilo hawakumaanisha bara lote bali eneo katika Tunisia ya leo tu. Asili yake ni kabila la "Afrig" lililoishi sehemu zile. Wakati huo Wagiriki wa Kale walitumia zaidi jina la Libya kwa ajili ya nchi kusini kwa Bahari ya Mediteraneo. Maeneo ya ndani kuelekea kusini mara nyingi yaliitwa kwa jina la "Ethiopia" linalomaanisha nchi ya watu weusiweusi (kwa Kigiriki "aithiops": aliyechomwa na jua).

hariri  fuatilia  

Nchi za Afrika

hariri  fuatilia  

Jamii

hariri  fuatilia  

Wasifu Uliochaguliwa

Idris I wa Libya
Idris I (Kiarabu: إدريس الأول idris-al-auwwal) (*12 Machi 1890 - 25 Mei 1983) alikuwa mfalme kwanza wa Libya kati ya 1951 hadi 1969. Jina lake la kiraia lilikuwa Muhamad Idris bin as-Sayyid ibn Muhamad as-Senussi (kiar.: محمد إدريس بن السيد المهدي ابن محمد السنوسي ). Alikuwa mjukuu wa Muhamad ibn Ali as-Senussi aliyeanzisha jumuiya ya Wasufi wa Senussi. Muhamad alirithi cheo cha babu yake. Alikubaliwa kama Emir wa Cyrenaika na Uingereza na Italia baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baada ya Italia kuvamia Libya aliongoza vita ya porini. Tangu 1951 aliongoza taifa jipya la Libya. 1969 alipinduliwa na wanajeshi chini ya uongozi wa Muammar al-Gaddafi. Alikufa Misri uhamishoni mwaka 1983.


hariri  fuatilia  

Makala iliyochaguliwa

Ziwa Nakuru ni mojawapo ya maziwa ya magadi katika mkoa wa Bonde la Ufa. Inapatikana kusini mwa mji wa Nakuru, katika eneo la kati nchini Kenya na ina zungukwa msitu wa wanyama wa Ziwa Nakuru. Wingi wa mwani katika ziwa hili huvutia kwa kiasi kikubwa ndege aina ya flamingo ambayo hupatikana sana katika ufuo ziwa hili. Ndege zingine pia hustawi katika eneo hili,na hata wanyama wengine wakubwa wa porini. Kiwango cha maji katika ziwa hili kilishuka kwa kasi kikubwa katika miaka ya 1990 lakini hivi karibuni kimeweza kurejea kiwango cha kale. Maana ya Nakuru ni "vumbi au Mahali pa vumbi" katika lugha ya Kimaasai. Mbuga ya wanyama ya ziwa Nakuru iliyoko karibu na mji wa Nakuru, ilianzishwa mwaka 1961. Ilianza ndogo, ikizingira ziwa hilo maarufu na maeneo ya milima yaliyokaribu. Na sasa imeongezwa kujumuisha sehemu kubwa ya maeneo ya savannah. Ziwa Nakuru imelindwa chini ya Mkataba wa Ramsar ya maeneo ya maji.


hariri  fuatilia  

Picha Iliyochaguliwa


Bustani ya Majorelle, Morocco.
(kupata bango)


hariri  fuatilia  

Je, wajua...?

...kwamba Ubuntu au "Obuntu" ni falsafa ya Kiafrika inayosisitiza mahusiano na ushirikiano wa jamii kama msingi wa maisha bora na amani katika jamii. Neno ubuntu limetoka kwenye lugha za Kizulu na KiXhosa za Afrika Kusini. Neno la Kihaya "Obuntu" au kwaKiswahili "utu" linabeba, kwa kiasi fulani, maana ya neno Obuntu.

hariri  fuatilia  

Masharika ya Wikimedia