Nenda kwa yaliyomo

Aruba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Pitio kulingana na tarehe 07:38, 13 Januari 2013 na DragonBot (majadiliano | michango) (r2.7.3) (Roboti: Imeongeza hsb:Aruba)
Aruba
Bendera ya Aruba Nembo ya Aruba
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: "Kisiwa chenye heri"
Wimbo wa taifa: Aruba Dushi Tera
Lokeshen ya Aruba
Mji mkuu Oranjestad
12°19′ N 70°1′ W
Mji mkubwa nchini Oranjestad
Lugha rasmi Kiholanzi, Papiamento1
Serikali
Ufalme wa kikatiba
Uhuru
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
193 km² ()
-
Idadi ya watu
 - 2006 kadirio
 - Msongamano wa watu
 
103.484 (ya 195)
571/km² (ya 18)
Fedha Florini ya Aruba (AWG2)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
AST (UTC-4)
(UTC)
Intaneti TLD .aw
Kodi ya simu +297

-



Aruba ni nchi ya kisiwani katika Bahari ya Karibi karibu na pwani la Venezuela. Inajitawala kama nchi mwanachama katika Ufalme wa Uholanzi lakini si sehemu ya Uholanzi.

Watu wa Aruba walielekea kwa uhuru wa kisiasa katika miaka ya 1980 na 1990. 1986 ilipata madaraka yote ya kujitawla chini ya taji la Uholanzi. Uhuru kamili ulipangwa kwa 1996 lakini serikali ya Aruba iliomba kutoendelea na mipango hii.

Wakazi ni mchanganyiko wa Maindio, Wazungu na pia Waafrika. Watumwa Waafrika hawakuwa wengi jinsi ilivyo kwenye visiwa vingi vya Karibi kwa sababu kisiwa haikuwa na mashamba mengi ya miwa kutokana na ukame wa mahali.

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Makala hii kuhusu maeneo ya Bahari ya Karibi bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Aruba kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.