Valentina Tereshkova
Mandhari
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/70/RIAN_archive_612748_Valentina_Tereshkova_%283-4_crop%29.jpg/220px-RIAN_archive_612748_Valentina_Tereshkova_%283-4_crop%29.jpg)
Valentina Vladimirovna Tereshkova (Kirusi Валентина Владимировна Терешкова) (* 6 Machi 1937) alikuwa mwanaanga kutoka Umoja wa Kisovieti na mwanamke wa kwanza aliyefika kwenye anga-nje.
Alikuwa mtoto wa mkulima aliyeendelea kusoma uhandisi akafaulu kupita mtihani kwa shule ya wanaanga mwaka 1962.
Tar. 16 Juni 1963 alirushwa kwa chombo cha angani Vostok 6 akazunguka dunia mara 49 akarudi duniani 19 Juni.