Ugiriki

nchi katika Ulaya Kusini-Mashariki

Ugiriki (pia: Uyunani; kwa Kigiriki cha kisasa: Ελλάδα, Ellada, au Ελλάς, Ellas) ni nchi ya Ulaya Kusini-Mashariki iliyopo kusini mwa rasi ya Balkani.

Ελληνική Δημοκρατία
Ellinikí Dimokratía

Demokrasia ya Ugiriki
Bendera ya Greece Nembo ya Greece
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Ελευθερία ή Θάνατος
(Eleftheria i thanatos - "Uhuru au mauti")
Wimbo wa taifa: Ύμνος εις την Ελευθερίαν - "Wimbo la Uhuru"
Lokeshen ya Greece
Mji mkuu Athens
38°00′ N 23°43′ E
Mji mkubwa nchini Athens
Lugha rasmi Kigiriki
Serikali Jamhuri
Katerina Sakellaropoulou (Κατερίνα Σακελλαροπούλου)
Kyriakos Mitsotakis (Κυριάκος Μητσοτάκης)
Uhuru
Ilitangazwa
Ilitambuliwa

25 Machi 1821
1829
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
131,957 km² (ya 95)
1.51
Idadi ya watu
 - 2021 kadirio
 - 2012 sensa
 - Msongamano wa watu
 
10,678,632 (ya 85)
10,816,286
77/km² (ya 120)
Fedha Euro ()2 (EUR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
EET (UTC+2)
EEST (UTC+3)
Intaneti TLD .gr 3
Kodi ya simu +30

-

1 Wananchi walikataza kurudi kwa ufalme tar. 8 Desemba 1974.
2 Prior to 2001: Greek Drachma.


Imepakana na Albania, Masedonia Kaskazini, Bulgaria na Uturuki. Upande wa kusini-magharibi na kusini-mashariki kuna pwani ndefu kwenye Bahari ya Mediteranea.

Jiografia

hariri

Kijiografia huwa na sehemu za Ugiriki bara, rasi ya Peloponesi upande wa kusini inayounganishwa kwa shingo ya nchi nyembamba, halafu visiwa vingi upande wa Bahari ya Aegean, Bahari ya Adria na kwenye Mediteranea yenyewe. Visiwa vikubwa zaidi ni Kreta, Euboea, Lesbo na Rhodos.

Historia

hariri
 
Parthenon, katika Akropoli ya Athens, ni kielelezo cha Ugiriki wa Kale.

Ugiriki ni nchi yenye historia ndefu na maarufu sana, hata inaitwa "nchi mama ya Ulaya" na kitovu cha Ustaarabu wa magharibi, kwa sababu ndipo vilipoanza demokrasia, falsafa ya magharibi, fasihi ya magharibi, historiografia, sayansi ya siasa, tafiti za sayansi na hisabati, tamthilia na michezo ya Olimpiki.

Ugiriki ni nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu 1981.

Lugha ya Kigiriki inaendelea kuandikwa kwa Alfabeti ya Kigiriki inayotumiwa tangu miaka 3000 iliyopita, lakini lugha yenyewe imebadilika. Wagiriki wa leo hawaelewi tena Kigiriki cha Kale moja kwa moja.

Wakazi wengi wanafuata dini ya Ukristo (93%), hasa katika Kanisa la Kiorthodoksi la Kigiriki (90%), halafu Waprotestanti na Wakatoliki. 2% ni Waislamu.

Tazama pia

hariri

Marejeo

hariri

Viungo vya nje

hariri


Nchi za Umoja wa Ulaya  
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
  Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ugiriki kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.