Michezo ya Olimpiki inafunguliwa jijini Paris nchini Ufaransa, Ijumaa jioni
Jiji la Paris linaanda tena michezo hii kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1924.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Hii itakuwa mara ya tatu kwa jiji hilo kuu la Ufaransa kuandaa Olimpiki, baada ya kufanya hivyo mara ya kwanza mwaka 1900, 1924 na sasa 2024.
Kinyume na miaka iliyopita, ufunguzi wa Michezo hii, utakuwa wa kipekee, hautafanyika uwanjani.
Sherehe za ufunguzi zitafanyika katika mto Seine, unaopita katikati ya jiji la Paris.
Wanamichezo 7,500 watapanda kwenye maboti 85 wakipita mbele ya mashabiki 300, 000 na wageni mashuhuri kutoka maeneo mbalimbali duniani wakiongozwa na rais Emmanuel Macron.
Michezo hiyo inayoanzwa Julai tarehe 26, itamalizika tarehe 11 mwezi Agosti.
Kutakuwa na Michezo 32 itakayoshindaniwa medali za dhahabu, Fedha na Shaba.