Egesipo

Mtakatifu Mkristo wa karne ya 2 na mwandishi wa historia

Egesipo (110 hivi – Yerusalemu, Israeli/Palestina, 180) alikuwa Myahudi aliyeongokea Ukristo akawa mwandishi wa vitabu mbalimbali ambavyo sehemu chache tu zimetufikia[1][2]. Muhimu zaidi ni masimulizi yake manyofu juu ya historia ya Kanisa kuanzia Mateso ya Yesu hadi wakati alipoishi mwenyewe, lakini aliandika pia dhidi ya uzushi.

Mwenyeji wa Mashariki ya Kati, aliishi miaka ishirini huko Roma chini ya Mapapa Aniseti, Soteri na Eleuteri [3].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Aprili[4].

Tazama pia

hariri

Tanbihi

hariri

Viungo vya nje

hariri
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.